13. Basi, kutakuwa na wakati mbayaambao hata mwenye busara atanyamaza.
14. Tafuteni kutenda mema na si mabaya,ili nyinyi mpate kuishinaye Mwenyezi-Mungu wa majeshiawe pamoja nanyi kama mnavyosema.
15. Chukieni uovu, pendeni wema,na kudumisha haki mahakamani.Yamkini Mwenyezi-Mungu wa majeshi atawafadhili watu wa Yosefu waliobaki.
16. Basi, Mwenyezi-Mungu, Mungu wa majeshi,naam, Mwenyezi-Mungu asema:“Patakuwa na kilio kila mahali mitaani;watu wataomboleza: ‘Ole! Ole!’Wakulima wataitwa waje kuomboleza,na mabingwa wa kuomboleza waje kufanya matanga.