Agano la Kale

Agano Jipya

2 Wafalme 4:30-34 Biblia Habari Njema (BHN)

30. Mwanamke akamwambia Elisha, “Kama Mwenyezi-Mungu aishivyo na kama wewe uishivyo, sitakuacha.” Basi Elisha akaondoka na kufuatana naye.

31. Gehazi akatangulia mbele, na alipofika akaweka fimbo ya Elisha juu ya uso wa mtoto, lakini hakukuonekana dalili yoyote ya uhai. Akarudi na kukutana na Elisha, akamwambia, “Kijana hakufufuka.”

32. Elisha alipofika, akaingia peke yake chumbani na kuona maiti ya kijana kitandani.

33. Basi, akafunga mlango na kumwomba Mwenyezi-Mungu.

34. Ndipo akajilaza juu ya mtoto, mdomo wake juu ya mdomo wa mtoto, na macho yake juu ya macho ya mtoto na mikono yake juu ya mikono ya mtoto. Na alipokuwa amekaa hivyo, mwili wa mtoto ukaanza kupata joto.

Kusoma sura kamili 2 Wafalme 4