Agano la Kale

Agano Jipya

2 Wafalme 4:29-33 Biblia Habari Njema (BHN)

29. Elisha akamwambia Gehazi, “Chukua fimbo yangu, uondoke mara moja. Usisimame njiani kumwamkia mtu yeyote, na mtu yeyote akikuamkia njiani, usipoteze wakati kurudisha salamu. Nenda moja kwa moja mpaka nyumbani na kuweka fimbo yangu juu ya mtoto.”

30. Mwanamke akamwambia Elisha, “Kama Mwenyezi-Mungu aishivyo na kama wewe uishivyo, sitakuacha.” Basi Elisha akaondoka na kufuatana naye.

31. Gehazi akatangulia mbele, na alipofika akaweka fimbo ya Elisha juu ya uso wa mtoto, lakini hakukuonekana dalili yoyote ya uhai. Akarudi na kukutana na Elisha, akamwambia, “Kijana hakufufuka.”

32. Elisha alipofika, akaingia peke yake chumbani na kuona maiti ya kijana kitandani.

33. Basi, akafunga mlango na kumwomba Mwenyezi-Mungu.

Kusoma sura kamili 2 Wafalme 4