Agano la Kale

Agano Jipya

2 Wafalme 3:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa mfalme Yehoshafati wa Yuda, Yoramu mwana wa Ahabu alianza kutawala Israeli, akatawala kutoka Samaria kwa muda wa miaka kumi na miwili.

2. Yoramu alitenda maovu mbele ya Mwenyezi-Mungu, lakini yeye hakuwa mbaya kama baba na mama yake; maana alibomolea mbali mnara wa Baali uliofanywa na baba yake.

3. Hata hivyo, Yoramu hakuacha dhambi kama mfalme Yeroboamu mwana wa Nebati aliyemtangulia ambaye alifanya dhambi na kuwafanya watu wa Israeli watende dhambi.

4. Mfalme Mesha wa Moabu alikuwa mfuga kondoo, na kila mwaka alitoa ushuru kwa mfalme wa Israeli wanakondoo laki moja na sufu ya kondoo laki moja.

5. Lakini Ahabu alipofariki, mfalme wa Moabu alimwasi.

6. Kwa hiyo mfalme Yoramu akaondoka Samaria, akakusanya jeshi lote la Israeli.

Kusoma sura kamili 2 Wafalme 3