Agano la Kale

Agano Jipya

2 Wafalme 21:22-26 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Alimwacha Mwenyezi-Mungu, Mungu wa babu zake, hakushika njia ya Mwenyezi-Mungu.

23. Baadaye watumishi wa Amoni walikula njama na kumwua katika ikulu yake.

24. Lakini watu wa Yuda wakawaua wote waliomuua Amoni. Kisha watu hao wa Yuda wakamtawaza Yosia mwanawe mahali pake.

25. Matendo mengine yote ya Amoni yameandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Yuda.

26. Amoni alizikwa kaburini katika bustani ya Uza; na Yosia mwanawe akatawala mahali pake.

Kusoma sura kamili 2 Wafalme 21