Agano la Kale

Agano Jipya

2 Samueli 4:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ishboshethi mwana wa Shauli, aliposikia kwamba Abneri ameuawa huko Hebroni, alivunjika moyo na watu wote wa Israeli walifadhaika.

2. Ishboshethi mwana wa Shauli, alikuwa na watu wawili waliokuwa viongozi wa kikosi cha uvamizi; mmoja aliitwa Baana na mwingine Rekabu. Hao walikuwa wana wa Rimoni, mtu wa kabila la Benyamini kutoka mji wa Be-erothi, (kwa maana Be-erothi pia ulikuwa mali ya kabila la Benyamini).

3. Wakazi wa Be-erothi walikimbilia Gitaimu, na wameishi huko kama wageni hadi leo.

Kusoma sura kamili 2 Samueli 4