Agano la Kale

Agano Jipya

2 Samueli 23:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Yafuatayo ni maneno ya mwisho ya Daudi. Ni ujumbe wa Daudi mwana wa Yese; ujumbe wa mtu ambaye Mungu alimfanya awe mkuu. Mungu wa Yakobo alimteua Daudi kuwa mfalme na maneno yake Waisraeli walifurahi kuyaimba.

2. “Roho ya Mwenyezi-Mungu imesema kwa njia yangu,aliyaweka maneno yake kinywani mwangu.

3. Mungu wa Israeli amesema,Mwamba wa Israeli ameniambia,‘Mtu anapowatawala watu kwa haki,atawalaye kwa kumcha Mungu,

4. yeye ni kama mwanga wa asubuhi,jua linapochomoza asubuhi isiyo na mawingu;naam, kama mvua inayootesha majani ardhini’.

5. Hivyo ndivyo Mungu alivyoujalia ukoo wangu.Maana amefanya nami agano la kudumu milele;agano kamili na thabiti.Naye atanifanikisha katika matakwa yangu yote.

Kusoma sura kamili 2 Samueli 23