1. Yafuatayo ni maneno ya mwisho ya Daudi. Ni ujumbe wa Daudi mwana wa Yese; ujumbe wa mtu ambaye Mungu alimfanya awe mkuu. Mungu wa Yakobo alimteua Daudi kuwa mfalme na maneno yake Waisraeli walifurahi kuyaimba.
2. “Roho ya Mwenyezi-Mungu imesema kwa njia yangu,aliyaweka maneno yake kinywani mwangu.
3. Mungu wa Israeli amesema,Mwamba wa Israeli ameniambia,‘Mtu anapowatawala watu kwa haki,atawalaye kwa kumcha Mungu,