Agano la Kale

Agano Jipya

2 Mambo Ya Nyakati 9:27-31 Biblia Habari Njema (BHN)

27. Basi Solomoni alifanya fedha katika Yerusalemu kuwa kitu cha kawaida kama mawe katika Yerusalemu, na mbao za mierezi zilipatikana kwa wingi kama mikuyu iliyomo Shefela.

28. Solomoni aliletewa farasi walionunuliwa kutoka Misri na nchi nyinginezo.

29. Matendo mengine ya Solomoni, kutoka mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha “Historia ya Nabii Nathani,” katika “Unabii wa Ahiya wa Shilo,” na katika “Maono ya Ido” mwonaji, ambayo yahusu pia Yeroboamu mwana wa Nebati.

30. Solomoni alitawala nchi yote ya Israeli kwa miaka arubaini.

31. Hatimaye Solomoni alifariki dunia na kuzikwa katika mji wa Daudi baba yake. Rehoboamu, mwanawe, akatawala mahali pake.

Kusoma sura kamili 2 Mambo Ya Nyakati 9