Agano la Kale

Agano Jipya

2 Mambo Ya Nyakati 9:22-28 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Mfalme Solomoni aliwapita wafalme wote duniani kwa mali na kwa hekima.

23. Nao wafalme wa nchi zote walikuwa na hamu ya kumwendea Solomoni ili kusikiliza hekima yake ambayo Mungu alikuwa amemjalia.

24. Kila mmoja wao alimletea zawadi: Vyombo vya fedha na vya dhahabu, mavazi na silaha manukato, farasi na nyumbu. Zawadi hizi alizipokea kila mwaka.

25. Mfalme Solomoni akawa na vibanda 4,000 vya kuwekea farasi na magari, na askari wapandafarasi 12,000 ambao aliwaweka katika miji yenye vituo vya magari ya farasi na katika Yerusalemu.

26. Aliwatawala wafalme wote waliokuwako kuanzia mto Eufrate, hadi nchi ya Wafilisti na hadi mpakani na Misri.

27. Basi Solomoni alifanya fedha katika Yerusalemu kuwa kitu cha kawaida kama mawe katika Yerusalemu, na mbao za mierezi zilipatikana kwa wingi kama mikuyu iliyomo Shefela.

28. Solomoni aliletewa farasi walionunuliwa kutoka Misri na nchi nyinginezo.

Kusoma sura kamili 2 Mambo Ya Nyakati 9