Agano la Kale

Agano Jipya

2 Mambo Ya Nyakati 6:36-42 Biblia Habari Njema (BHN)

36. “Ikiwa watatenda dhambi dhidi yako, maana hakuna mtu asiyetenda dhambi, na ukiwakasirikia na kuwaacha washindwe na adui, hata wapelekwe mateka mpaka nchi ya mbali au ya karibu;

37. kama watakapokuwa huko uhamishoni watajirudi kwa roho yao yote na kwa moyo wao wote na kutubu na kukuomba msamaha, wakisema, ‘Tumetenda dhambi; tumepotoka na kufanya maovu’;

38. pia kama watatubu kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote wakati watakapokuwa katika nchi ya uhamisho, na kama watakuomba wakielekea nchi yao ambayo uliwapatia babu zao, mji huu ambao uliuchagua na nyumba hii ambayo nimeijenga kwa ajili ya jina lako;

39. basi, nakusihi usikie huko mbinguni uliko sala yao na maombi yao na uwapatie haki zao, uwasamehe watu wako ambao wametenda dhambi dhidi yako.

40. “Sasa ee Mungu wangu, tuangalie na upokee maombi tutakayoomba mahali hapa.

41. Sasa inuka ee Bwana Mungu,uingie mahali pako pa kupumzikawewe pamoja na sanduku la agano la nguvu zako.Makuhani wako ee Bwana Mungu, wapate wokovu,na watakatifu wako wafurahie wema wako.

42. Ee Bwana Mungu, usimpige kisogo masiha wako.Kumbuka fadhili zako kwa mtumishi wako Daudi.”

Kusoma sura kamili 2 Mambo Ya Nyakati 6