Agano la Kale

Agano Jipya

2 Mambo Ya Nyakati 5:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Hivyo, Solomoni akamaliza kazi zote zilizohusu nyumba ya Mwenyezi-Mungu. Kisha Solomoni akaleta mali yote Daudi baba yake aliyokuwa ameiweka wakfu, yaani: Fedha, dhahabu na vyombo; akaiweka katika hazina za nyumba ya Mungu.

2. Basi mfalme Solomoni akawakutanisha Yerusalemu wazee na viongozi wote wa makabila na wa koo za Israeli ili waliondoe sanduku la agano la Mwenyezi-Mungu kutoka katika mji wa Daudi, yaani Siyoni.

3. Ndipo wote walipokutana mbele ya mfalme katika sikukuu ya mwezi wa saba.

4. Baada ya wazee wote wa Israeli kuwasili, Walawi walilibeba sanduku la agano,

5. Walawi na makuhani walilihamisha sanduku la agano na hema la mkutano na vyombo vitakatifu vyote vilivyokuwa humo hemani.

6. Mfalme Solomoni na mkutano wa Israeli wakakusanyika mbele ya sanduku la agano nao wakatoa sadaka za ng'ombe na kondoo wasiohesabika.

Kusoma sura kamili 2 Mambo Ya Nyakati 5