Agano la Kale

Agano Jipya

2 Mambo Ya Nyakati 33:21-25 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Amoni alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala Yuda; alitawala miaka miwili huko Yerusalemu.

22. Alitenda maovu mbele ya Mwenyezi-Mungu, kama vile Manase baba yake alivyofanya. Pia alitoa sadaka na kutumikia sanamu ambazo Manase baba yake alichonga.

23. Naye hakujinyenyekesha mbele za Mwenyezi-Mungu, kama alivyofanya Manase, lakini yeye aliongeza kutenda makosa zaidi.

24. Baadaye watumishi wake walikula njama na kumuua katika ikulu yake.

25. Lakini watu wa Yuda wakawaua hao wote waliokula njama dhidi ya Amoni; kisha wakamfanya Yosia, mwanawe kuwa mfalme badala yake.

Kusoma sura kamili 2 Mambo Ya Nyakati 33