1. Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala. Alitawala kwa muda wa miaka arubaini huko Yerusalemu. Mama yake alikuwa Sibia kutoka Beer-sheba.
2. Wakati wote kuhani Yehoyada alipokuwa hai Yoashi alitenda mema mbele ya Mwenyezi-Mungu.
3. Yehoyada akamwoza wake wawili, nao wakamzalia watoto wa kiume na wa kike.
4. Baadaye Yoashi aliamua kurekebisha nyumba ya Mwenyezi-Mungu.