Agano la Kale

Agano Jipya

2 Mambo Ya Nyakati 24:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala. Alitawala kwa muda wa miaka arubaini huko Yerusalemu. Mama yake alikuwa Sibia kutoka Beer-sheba.

2. Wakati wote kuhani Yehoyada alipokuwa hai Yoashi alitenda mema mbele ya Mwenyezi-Mungu.

3. Yehoyada akamwoza wake wawili, nao wakamzalia watoto wa kiume na wa kike.

4. Baadaye Yoashi aliamua kurekebisha nyumba ya Mwenyezi-Mungu.

Kusoma sura kamili 2 Mambo Ya Nyakati 24