Agano la Kale

Agano Jipya

2 Mambo Ya Nyakati 10:12-19 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Basi katika siku ya tatu Yeroboamu pamoja na watu wote wakarudi kwa Rehoboamu kama alivyokuwa amewaagiza.

13. Naye mfalme Rehoboamu akawajibu kwa ukali, akapuuza shauri la wazee,

14. na kufuata shauri la vijana wenzake. Basi akasema, “Baba yangu aliwatwika mzigo mzito, lakini mimi nitaufanya kuwa mzito zaidi. Baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, lakini mimi nitawapiga kwa mijeledi yenye miiba”

15. Hivyo mfalme hakuwajali watu kwa sababu jambo hili lilisababishwa na Mungu ili Mwenyezi-Mungu atimize neno lake alilomwambia Yeroboamu, mwana wa Nebati kwa njia ya Ahiya wa Shilo.

16. Lakini watu wote wa Israeli walipoona kwamba mfalme hakuwajali walimwambia,“Tuna sehemu gani kwa Daudi?Hatuna urithi katika mwana wa Yese.Kila mmoja na arudi nyumbani kwake, enyi watu wa Israeli.Itunze nyumba yako mwenyewe, ee Daudi.”Hivyo watu wote wa Israeli wakarudi makwao.

17. Lakini Rehoboamu alitawala watu wa Israeli waliokaa katika miji ya Yuda.

18. Kisha mfalme Rehoboamu alipomtuma Hadoramu aliyekuwa mnyapara mkuu wa kazi za kulazimishwa, watu wa Israeli walimpiga mawe, wakamuua. Ndipo Rehoboamu alipopanda gari lake haraka akakimbilia Yerusalemu.

19. Hivyo, watu wa Israeli wamekuwa katika hali ya maasi dhidi ya utawala wa ukoo wa Daudi mpaka leo.

Kusoma sura kamili 2 Mambo Ya Nyakati 10