Agano la Kale

Agano Jipya

2 Mambo Ya Nyakati 10:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Basi, Rehoboamu akaenda Shekemu, ambako Waisraeli wote walikuwa wamekusanyika ili kumtawaza awe mfalme.

2. Naye Yeroboamu mwana wa Nebati alipopata habari kuhusu tendo hilo (wakati huo alikuwa bado anaishi Misri alikokwenda alipomkimbia Solomoni) alitoka Misri.

3. Lakini Waisraeli walituma ujumbe na kumwita. Kisha, yeye pamoja na Waisraeli wote walimwendea Rehoboamu na kumwambia,

4. “Baba yako alitutwika mzigo mzito. Basi, utupunguzie mzigo huo, nasi tutakutumikia.”

5. Rehoboamu akawajibu, “Rudini kwangu baada ya siku tatu.” Basi wakaondoka.

Kusoma sura kamili 2 Mambo Ya Nyakati 10