Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wafalme 8:40-45 Biblia Habari Njema (BHN)

40. ili wakutii wakati wote wanapoishi katika nchi uliyowapa babu zetu.

41. “Vivyo hivyo, wakati mgeni asiye mmoja wa watu wako Israeli akija kutoka nchi ya mbali kwa ajili ya jina lako

42. (maana watu wa mataifa mengine watasikia sifa zako na kuhusu nguvu na uwezo wako), mtu huyo akija na kuomba katika nyumba hii,

43. nakusihi umsikie kutoka huko mbinguni, na umjalie huyo mgeni yote atakayokuomba; kusudi watu wote ulimwenguni wapate kujua jina lako na kukutii kama wafanyavyo watu wako, Israeli, na wapate kufahamu kwamba nyumba hii ambayo nimeijenga, inajulikana kwa jina lako.

44. “Watu wako wakienda vitani kupigana na adui yao kokote kule utakakowapeleka, nao wakikuomba wakielekea mji uliouchagua na nyumba niliyoijenga kwa ajili ya jina lako,

45. nakusihi usikie sala yao na maombi yao huko mbinguni, uwapatie ushindi vitani.

Kusoma sura kamili 1 Wafalme 8