Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wafalme 8:11-14 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Nao makuhani walishindwa kuhudumu kwa sababu ya wingu hilo; kwa kuwa utukufu wa Mwenyezi-Mungu uliijaza nyumba ya Mwenyezi-Mungu.

12. Ndipo Solomoni akasema,“Mwenyezi-Mungu alisema kwamba,atakaa katika giza nene.

13. Hakika, nimekujengea nyumba ya kukaa,mahali pa makao yako ya milele.”

14. Kisha, Solomoni akaigeukia jumuiya yote ya Waisraeli wakiwa wamesimama, akawabariki,

Kusoma sura kamili 1 Wafalme 8