Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wafalme 15:7-12 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Matendo mengine ya Abiya, na yote aliyoyafanya yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Nyakati ya Wafalme wa Yuda. Abiya na Yeroboamu waliishi katika hali ya vita.

8. Mwishowe, Abiya alifariki na kuzikwa katika mji wa Daudi na mwanawe Asa akatawala mahali pake.

9. Mnamo mwaka wa ishirini wa utawala wa Yeroboamu, mfalme wa Israeli, Asa alianza kutawala huko Yuda.

10. Alitawala kwa muda wa miaka arubaini na mmoja. Mama yake alikuwa Maaka, binti Absalomu.

11. Mfalme Asa alitenda yaliyo mema mbele ya Mwenyezi-Mungu kama alivyofanya Daudi babu yake.

12. Aliwafukuza nchini wale wafiraji wa kidini, akaziondoa sanamu zote ambazo babu zake walikuwa wamezitengeneza.

Kusoma sura kamili 1 Wafalme 15