Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wafalme 15:6-18 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Kulikuwako vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu wakati wote alipokuwa mtawala.

7. Matendo mengine ya Abiya, na yote aliyoyafanya yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Nyakati ya Wafalme wa Yuda. Abiya na Yeroboamu waliishi katika hali ya vita.

8. Mwishowe, Abiya alifariki na kuzikwa katika mji wa Daudi na mwanawe Asa akatawala mahali pake.

9. Mnamo mwaka wa ishirini wa utawala wa Yeroboamu, mfalme wa Israeli, Asa alianza kutawala huko Yuda.

10. Alitawala kwa muda wa miaka arubaini na mmoja. Mama yake alikuwa Maaka, binti Absalomu.

11. Mfalme Asa alitenda yaliyo mema mbele ya Mwenyezi-Mungu kama alivyofanya Daudi babu yake.

12. Aliwafukuza nchini wale wafiraji wa kidini, akaziondoa sanamu zote ambazo babu zake walikuwa wamezitengeneza.

13. Alimvua Maaka, mama yake, cheo chake cha mama malkia, kwa sababu alitengeneza sanamu ya Ashera, mungu wa kike, na hiyo sanamu akaivunjavunja na kuiteketeza kwenye bonde la Kidroni.

14. Lakini mahali pa juu pa kutambikia miungu hapakuharibiwa; hata hivyo, yeye alikuwa na moyo mwaminifu kwa Mwenyezi-Mungu maisha yake yote.

15. Alirudisha nyumbani mwa Mwenyezi-Mungu vyombo vyote vilivyokuwa vimewekwa wakfu na baba yake, pamoja na vile vyake yeye mwenyewe: Vyombo vya fedha, dhahabu na vyombo vinginevyo.

16. Mfalme Asa wa Yuda, na mfalme Baasha wa Israeli, walikuwa na vita kati yao wakati wote walipokuwa wakitawala.

17. Baasha, mfalme wa Israeli, aliishambulia nchi ya Yuda na kuanza kuujenga Rama ili apate kuzuia mtu yeyote asitoke wala asiingie kwa Asa, mfalme wa Yuda.

18. Ndipo mfalme Asa akachukua fedha na dhahabu yote iliyobaki katika hazina ya nyumba ya Mwenyezi-Mungu na katika hazina ya ikulu, akawapa watumishi wake, akawatuma Damasko kwa Ben-hadadi mwana wa Tabrimoni, mjukuu wa Hezioni, mfalme wa Aramu, akasema,

Kusoma sura kamili 1 Wafalme 15