Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wafalme 14:28-31 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Kila wakati mfalme alipokwenda katika nyumba ya Mwenyezi-Mungu, walinzi walizibeba ngao hizo, na baadaye wakazirudisha katika chumba cha ulinzi.

29. Matendo mengine ya mfalme Rehoboamu, na yote aliyoyafanya, yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Nyakati ya Wafalme wa Yuda.

30. Daima kulikuwako vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.

31. Hatimaye, Rehoboamu alifariki na kuzikwa kwenye makaburi ya wazee wake, katika mji wa Daudi. Mama yake aliitwa Naama kutoka Amoni, na Abiyamu mwanawe akatawala mahali pake.

Kusoma sura kamili 1 Wafalme 14