Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wafalme 10:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Malkia wa Sheba aliposikia sifa za Solomoni, kwa sababu ya jina la Mwenyezi-Mungu, alimwendea Solomoni ili kumjaribu kwa maswali magumu.

2. Aliwasili akiwa amefuatana na msafara wa watu pamoja na ngamia waliobeba manukato, zawadi nyingi sana na vito vya thamani.

3. Naye Solomoni akayajibu maswali yote; hapakuwa na swali lolote lililomshinda.

Kusoma sura kamili 1 Wafalme 10