7. Mwenyezi-Mungu huwafanya baadhi wawe maskini,na baadhi wawe matajiri.Wengine huwashusha,na wengine huwakweza.
8. Huwainua maskini toka mavumbini;huwanyanyua wahitaji toka majivuni,akawaketisha pamoja na wakuu,na kuwarithisha viti vya heshima.Maana, minara ya dunia ni ya Mwenyezi-Mungu;yeye ameisimika dunia juu ya minara yake.
9. “Maisha ya waaminifu wake huyalinda,lakini maisha ya waovu huyakatilia mbali gizani.Maana, binadamu hapati ushindi kwa nguvu zake.
10. Maadui wa Mwenyezi-Mungu watavunjwa vipandevipande;atanguruma dhidi yao kama radi mbinguni.Mwenyezi-Mungu ataihukumu dunia yote;atampa nguvu mfalme wakeataukuza uwezo wa mteule wake.”
11. Kisha, Elkana akarudi nyumbani Rama. Lakini mtoto Samueli akabaki Shilo kumtumikia Mwenyezi-Mungu chini ya uongozi wa kuhani Eli.
12. Watoto wa kiume wa Eli walikuwa walaghai sana. Hawakumjali Mwenyezi-Mungu