Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 9:35-44 Biblia Habari Njema (BHN)

35. Yeieli alikuwa mwanzilishi wa mji wa Gibeoni ambamo aliishi yeye pamoja na mkewe, jina lake Maaka.

36. Mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Abdoni, naye alifuatiwa na Zuri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,

37. Gedori, Ahio, Zekaria na Miklothi.

38. Miklothi alimzaa Shimeamu. Wazawa wao waliishi Yerusalemu karibu na jamaa nyingine za koo zao.

39. Neri alimzaa Kishi, naye Kishi akamzaa Shauli. Shauli alikuwa na wana wanne: Yonathani, Malki-shua, Abinadabu na Eshbaali.

40. Yonathani alimzaa Merib-baali, Merib-baali akamzaa Mika.

41. Mika alikuwa na wana wanne: Pithoni, Meleki, Tarea na Ahazi.

42. Ahazi alimzaa Yara, Yara akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa,

43. Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Refaya, Refaya akamzaa Eleasa, naye Eleasa akamzaa Aseli.

44. Aseli alikuwa na wana sita: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hamani. Hawa wote walikuwa wana wa Aseli.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 9