Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 8:23-40 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Abdoni, Zikri, Hanani,

24. Hanania, Elamu, Anthothiya,

25. Ifdeya na Penueli walikuwa wazawa wa Shashaki.

26. Shamsherai, Sheharia, Athalia,

27. Yaareshia, Elia na Zikri walikuwa baadhi ya wazawa wa Yerohamu.

28. Hao ndio waliokuwa wakuu wa koo zao kulingana na vizazi vyao. Walikuwa wakuu na waliishi Yerusalemu.

29. Yeieli, alikuwa mwanzilishi wa mji wa Gibeoni. Mkewe alikuwa Maaka.

30. Mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Abdoni. Wanawe wengine ni Zuri, Kishi, Baali, Nadabu,

31. Gedori, Ahio, Zekeri,

32. na Miklothi baba yake Shimea. Hawa pia waliishi Yerusalemu karibu na watu wengine wa ukoo wao.

33. Neri alimzaa Kishi, Kishi akamzaa Shauli. Shauli alikuwa na wana wanne: Yonathani, Malki-shua, Abinadabu na Eshbaali.

34. Yonathani alimzaa Merib-baali, na Merib-baali akamzaa Mika.

35. Mika alikuwa na wana wanne: Pithoni, Meleki, Terea na Ahazi.

36. Ahazi alimzaa Yehoada. Naye Yehoada aliwazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri. Zimri alimzaa Mosa.

37. Mosa alimzaa Binea, aliyemzaa Rafa, aliyemzaa Eleasa, naye Eleasa akamzaa Aseli.

38. Wana wa Aseli walikuwa sita: Majina yao ni Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Wote hawa walikuwa wana wa Aseli.

39. Nao wana wa Esheki, nduguye Aseli, walikuwa watatu. Mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Ulamu, wa pili Yeushi na wa tatu Elifeleti.

40. Wana wa Ulamu walikuwa watu mashujaa sana wa vita, na wapiga upinde hodari. Alikuwa na wana na wajukuu wengi, jumla150. Hao wote waliotajwa hapo juu walikuwa wa ukoo wa Benyamini.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 8