Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 7:13-19 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Naftali alikuwa na wana wanne: Yaasieli, Guni, Yereri na Shalumu. Hao walikuwa wazawa wa Bilha.

14. Manase alikuwa na wana wawili kutokana na suria wake Mwaramu: Asrieli na Makiri. Makiri alikuwa baba yake Gileadi.

15. Makiri aliwazaa Hupimu na Shupimu. Jina la dada yake lilikuwa Maaka. Mwana wa pili wa Makiri alikuwa Selofehadi. Selofehadi alikuwa na mabinti peke yake.

16. Maaka mkewe Makiri, alizaa mwana jina lake Pereshi. Jina la nduguye Pereshi lilikuwa Shereshi. Wanawe Shereshi walikuwa Ulamu na Rakemu.

17. Rakemu alimzaa Bedani. Hawa wote ni wazawa wa Gileadi, mwana wa Makiri, mjukuu wa Manase.

18. Hamo-lekethi, dada yake Gileadi, aliwazaa Ishhodi, Abiezeri na Mala.

19. Wana wa Shemida walikuwa Ahiani, Shekemu, Liki na Aniamu.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 7