Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 6:74-81 Biblia Habari Njema (BHN)

74. Katika kabila la Asheri walipewa: Mashali pamoja na malisho yake, Abdoni pamoja na malisho yake,

75. Hukoki pamoja na malisho yake, na Rehobu na malisho yake.

76. Katika kabila la Naftali: Kedeshi katika Galilaya pamoja na malisho yake, Hamoni pamoja na malisho yake na Kiriathaimu pamoja na malisho yake.

77. Jamaa za Merari zilizosalia, zilipewa miji ifuatayo pamoja na malisho yake kandokando ya miji hiyo: Katika kabila la Zebuluni walipewa Rimono pamoja na malisho yake na Tabori pamoja na malisho yake.

78. Katika kabila la Reubeni, mashariki ya mto Yordani karibu na mji wa Yeriko walipewa Bezeri ulioko katika nyanda za juu pamoja na malisho yake, Yahasa pamoja na malisho yake,

79. Kedemothi pamoja na malisho yake na Mefaathi pamoja na malisho yake.

80. Katika kabila la Gadi walipewa Ramothi katika Gileadi pamoja na malisho yake, Mahanaimu pamoja na malisho yake,

81. Heshboni pamoja na malisho yake na Yazeri pamoja na malisho yake.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 6