Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 6:49-56 Biblia Habari Njema (BHN)

49. Aroni na wazawa wake ndio waliokuwa wakitoa tambiko juu ya madhabahu ya tambiko za kuteketezwa na pia juu ya madhabahu ya kufukizia ubani. Walifanya kazi zote zilizohusika na mahali patakatifu sana ili kuifanyia Israeli upatanisho. Haya yote waliyafanya kulingana na maagizo aliyotoa Mose, mtumishi wa Mungu.

50. Wafuatao ndio wazawa wa Aroni: Aroni alimzaa Eleazari, Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,

51. Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi, Uzi akamzaa Serahia,

52. Serahia akamzaa Merayothi, Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,

53. Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi.

54. Yafuatayo ndiyo makazi yao kulingana na mipaka yake: Wazawa wa Aroni katika jamaa ya Wakohathi kulingana na kura yao,

55. hao walipewa mji wa Hebroni katika nchi ya Yuda na malisho kandokando yake.

56. Lakini mashamba ya mjini pamoja na malisho yake alipewa Kalebu mwana wa Yefune.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 6