Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 6:32-47 Biblia Habari Njema (BHN)

32. Walifanya kazi yao ya kuimba mbele ya hema takatifu la mkutano hadi wakati mfalme Solomoni alipojenga hekalu la Mwenyezi-Mungu huko Yerusalemu. Waliutekeleza wajibu wao barabara, kwa zamu.

33. Zifuatazo ni koo za wale ambao walitoa huduma hizo: Ukoo wa Kohathi: Hemani, kiongozi wa kundi la kwanza la waimbaji, alikuwa mwana wa Yoeli. Ukoo wake kutokana na Israeli ni kama ifuatavyo: Hemani, mwana wa Yoeli, mwana wa Samueli,

34. mwana wa Elkana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elieli, mwana wa Toa,

35. mwana wa Zufu, mwana wa Elkana, mwana wa Mahathi, mwana wa Amasai,

36. mwana wa Elkana, mwana wa Yoeli, mwana wa Azaria, mwana wa Sefania,

37. mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora,

38. mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, mwana wa Israeli.

39. Asafu, ndugu yake alikuwa upande wake wa kulia. Ukoo wake kutokana na Lawi: Asafu, mwana wa Berekia, mwana wa Shimea,

40. mwana wa Mikaeli, mwana wa Baaseya, mwana wa Malkiya,

41. mwana wa Ethni, mwana wa Zera, mwana wa Adaya,

42. mwana wa Ethani, mwana wa Zima, mwana wa Shimei,

43. mwana wa Yahathi, mwana wa Gershomu, mwana wa Lawi.

44. Ethani wa ukoo wa Merari, alikuwa kiongozi wa kundi la tatu la waimbaji. Ukoo wake kutokana na Lawi ni kama ifuatavyo: Ethani, mwana wa Kishi, mwana wa Abdi, mwana wa Maluki,

45. mwana wa Hashabia, mwana wa Amazia, mwana wa Hilkia,

46. mwana wa Amsi, mwana wa Bani, mwana wa Shemeri,

47. mwana wa Mahli, mwana wa Mushi, mwana wa Merari, mwana wa Lawi.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 6