Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 6:14-27 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Azaria alimzaa Seraya, Seraya alimzaa Yehosadaki;

15. Yehosadaki alikwenda uhamishoni wakati Mwenyezi-Mungu alipowapeleka uhamishoni watu wa Yuda na Yerusalemu kwa kuutumia mkono wa mfalme Nebukadneza.

16. Lawi alikuwa na wana watatu: Gershomu, Kohathi na Merari.

17. Kila mmoja wao pia alikuwa na wana. Gershomu aliwazaa Libni na Shimei;

18. Kohathi aliwazaa Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli;

19. naye Merari aliwazaa Mahli na Mushi. Hizi ndizo jamaa za Walawi kulingana na koo zao.

20. Wafuatao ndio wazawa wa Gershomu kutoka kizazi hadi kizazi: Gershomu alimzaa Libni, Libni akamzaa Yahathi, Yahathi akamzaa Zima,

21. Zima akamzaa Yoa, Yoa akamzaa Ido, Ido akamzaa Zera, Zera akamzaa Yeatherai.

22. Hawa ndio wazawa wa Kohathi kutoka kizazi hadi kizazi: Kohathi alimzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Kora, Kora akamzaa Asiri,

23. Asiri akamzaa Elkana, Elkana akamzaa Ebiasafu, Ebiasafu akamzaa Asiri,

24. Asiri akamzaa Tahathi, Tahathi akamzaa Urieli, Urieli akamzaa Usia, Usia akamzaa Shauli.

25. Wana wa Elkana walikuwa wawili: Amasai na Ahimothi.

26. Na hawa ndio wazawa wa Ahimothi: Ahimothi alimzaa Elkana, Elkana akamzaa Sofai, Sofai akamzaa Nahathi,

27. Nahathi akamzaa Eliabu, Eliabu akamzaa Yerohamu, Yerohamu akamzaa Elkana.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 6