Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 4:26-38 Biblia Habari Njema (BHN)

26. Mishma alimzaa Hamueli, aliyemzaa Zakuri, na Zakuri akamzaa Shimei.

27. Shimei alikuwa na wana kumi na sita na binti sita, lakini ndugu zake hawakuwa na wana wengi, na jamii yake pia haikuongezeka kama kabila la Yuda.

28. Miji walimokuwa wakiishi ilikuwa Beer-sheba, Molada, Hasar-shuali,

29. Bilha, Ezemu, Toladi;

30. Bethueli, Horma, Siklagi,

31. Beth-markabothi, Hazar-susimu, Beth-biri na Shaaraimu. Hiyo ndiyo miji yao mpaka wakati wa utawala wa mfalme Daudi.

32. Pia, waliishi katika miji mingine mitano: Etamu, Aini, Rimoni, Tokeni na Ashani,

33. pamoja na vijiji kandokando ya miji hiyo huko Baali. Hayo ndiyo yaliyokuwa makao yao, nao waliweka kumbukumbu ya nasaba yao.

34. Watu wafuatao walikuwa wakuu wa koo zao: Meshobabu, Yamleki, Yosha mwana wa Amazia,

35. Yoeli, Yehu (mwana wa Yoshibia, mwana wa Seraya, mwana wa Asieli.)

36. Eliehonai, Yaakoba, Yeshohaya, Asaya, Adieli, Yesimieli, Benaya,

37. Ziza (mwana wa Shifi, mwana wa Aloni, mwana wa Yedaya, mwana wa Shimri na mwana wa Shemaya).

38. Jamaa zao waliendelea kuongezeka kwa wingi sana. Hawa waliotajwa majina ni wakuu katika jamaa zao na koo zao ziliongezeka sana.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 4