Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 26:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Haya ndiyo makundi ya Walawi waliofanya kazi za ubawabu. Kutoka katika ukoo wa Kora, alikuwa Meshelemia mwana wa Kore wa jamaa ya Asafu.

2. Yeye alikuwa na wana saba: Zekaria mzaliwa wake wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne,

3. Elamu wa tano, Yohanani wa sita na Eliehoenai wa saba.

4. Pia kulikuwa na Obed-edomu, ambaye Mungu alimbariki kwa kumpa wana wanane: Shemaya mzaliwa wake wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, Sakari wa nne, Nethaneli wa tano,

5. Amieli wa sita, Isakari wa saba na Peulethai wa nane.

6. Naye mwanawe Shemaya alipata wana waliokuwa na mamlaka juu ya jamaa ya baba yao, kwa sababu walikuwa wanaume wenye uwezo mkubwa.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 26