Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 25:7-14 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Idadi yao pamoja na wale ndugu zao Walawi waliofundishwa kumwimbia Mwenyezi-Mungu, wote waliokuwa stadi, ilikuwa 288.

8. Wote, wakubwa kwa wadogo, waalimu kwa wanafunzi, walitumia kura katika kupanga kazi zao.

9. Kura ya 1 ilimwangukia Yosefu wa jamaa ya Asafu; ya 2 Gedalia pamoja na ndugu zake na wanawe kumi na wawili;

10. ya 3 Zakuri pamoja na wanawe na ndugu zake kumi na wawili;

11. ya 4 ilimwangukia Seri pamoja na wanawe na ndugu zake kumi na wawili;

12. ya 5 Nethania; pamoja na wanawe na ndugu zake kumi na wawili;

13. ya 6 Bukia; pamoja na wanawe na ndugu zake kumi na wawili;

14. ya 7 Asharela; pamoja na wanawe na ndugu zake kumi na wawili;

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 25