9. ya 5 Malkia; ya 6 Miyamini;
10. ya 7 Hakosi; ya 8 Abiya;
11. ya 9 Yeshua; ya 10 Shekania;
12. ya 11 Eliashibu; ya 12 Yakimu;
13. ya 13 Hupa; ya 14 Yeshebeabu;
14. ya 15 Bilga; ya 16 Imeri;
15. ya 17 Heziri; ya 18 Hapisesi;
16. ya 19 Pethahia; ya 20 Yehezkeli;
17. ya 21 Yakini; ya 22 Gamuli;
18. ya 23 Delaya; na ya 24 Maazia.
19. Hawa waliandikishwa kulingana na kazi zao kuingia katika nyumba ya Mwenyezi-Mungu kutoa huduma, kadiri ya utaratibu waliowekewa na Aroni babu yao, kama alivyoamriwa na Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli.
20. Hawa ndio wazawa wengine wa Lawi: Mmoja wa wazawa wa Amramu alikuwa Shubaeli; wa Shubaeli alikuwa Yedeya.
21. Mmoja wa wazawa wa Rehabia alikuwa Ishio kiongozi wa ukoo.
22. Mmoja wa wazawa wa Ishio alikuwa Shelomithi na wa wazawa wa Shelomithi alikuwa Yahathi.
23. Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria wa kwanza, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, Yakameamu wa nne.