Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 23:2-16 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Mfalme Daudi aliwakusanya wakuu wote wa Israeli, makuhani na Walawi.

3. Walawi wote wanaume wenye umri wa miaka thelathini na zaidi, wakahesabiwa. Jumla yao ilikuwa 38,000.

4. Hao, Daudi aliwagawanya: 24,000 kati yao wawe wasimamizi wa kazi ya nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu, 6,000 wawe maofisa na waamuzi,

5. 4,000 wawe mabawabu, na 4,000 wawe waimbaji, wakimsifu Mwenyezi-Mungu kwa ala za muziki alizotengeneza mfalme mwenyewe kwa madhumuni hayo.

6. Daudi aliwagawanya Walawi katika makundi matatu kulingana na koo za kabila la Lawi: Ukoo wa Gershoni, ukoo wa Kohathi na ukoo wa Merari.

7. Wana wa Gershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.

8. Ladani alikuwa na wana watatu: Yehieli mkuu wao, Zethamu na Yoeli.

9. Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomithi, Hazieli na Harani. Hawa walikuwa viongozi wa ukoo wa Ladani.

10. Wana wa Shimei walikuwa viongozi wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.

11. Yahathi ndiye aliyekuwa mkuu wao, akifuatiwa na Ziza. Lakini Yeushi na Beria, kwa vile hawakuwa na wana wengi, walichukuliwa na ukoo mmoja.

12. Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.

13. Wana wa Amramu walikuwa Aroni na Mose. Aroni aliteuliwa awe akiweka wakfu vyombo vitakatifu kabisa, pia wazawa wake daima wafukizie ubani mbele za Mwenyezi-Mungu, wakimtumikia na kuwabariki watu katika jina la Mwenyezi-Mungu milele.

14. Lakini wana wa Mose, mtu wa Mungu, hutajwa miongoni mwa kabila la Lawi.

15. Wana wa Mose walikuwa Gershomu na Eliezeri.

16. Aliyekuwa mkuu miongoni mwa wana wa Gershomu ni Shebueli.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 23