Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 2:36-50 Biblia Habari Njema (BHN)

36. Atai alimzaa Nathani, Nathani akamzaa Zabadi.

37. Zabadi akamzaa Eflali, Eflali akamzaa Obedi,

38. Obedi akamzaa Yehu, Yehu akamzaa Azaria,

39. Azaria akamzaa Helesi, Helesi akamzaa Eleasa,

40. Eleasa akamzaa Sismai, Sismai akamzaa Shalumu,

41. Shalumu akamzaa Yekamia, na Yekamia akamzaa Elishama.

42. Mzaliwa wa kwanza wa Kalebu, nduguye Yerameeli, aliitwa Mesha. Mesha alimzaa Zifu, Zifu akamzaa Maresha, Maresha akamzaa Hebroni.

43. Hebroni alikuwa na wana wanne: Kora, Tapua, Rekemu na Shema.

44. Shema alikuwa baba yake Rahamu na babu yake Rekemu. Rekemu nduguye Shema alimzaa Shamai,

45. Shamai akamzaa Maoni, na Maoni akamzaa Beth-suri.

46. Kalebu alikuwa na suria, jina lake Efa. Huyu alimzalia wana wengine watatu: Harani, Mosa na Gazezi. Harani alimzaa Gazezi.

47. Yadai alikuwa na wana sita: Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa na Shaafu.

48. Kalebu alikuwa na suria mwingine jina lake Maaka. Huyu alimzalia wana wawili: Sheberi na Tirhana.

49. Maaka alimzalia Kalebu wana; Shaafu mwanzilishi wa mji wa Madmana, na Sheva, mwanzilishi wa mji wa Makbena na Gibea. Kalebu alikuwa pia na binti, jina lake Aksa.

50. Kalebu alikuwa na wazawa wengine pia kwa mkewe Efratha. Huri, mzaliwa wake wa kwanza, alikuwa na wana watatu: Shobali, mwanzilishi wa mji wa Kiriath-yearimu,

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 2