Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 2:30-40 Biblia Habari Njema (BHN)

30. Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu; lakini Seledi alifariki bila watoto.

31. Apaimu alikuwa na mwana mmoja aliyeitwa Ishi. Ishi alimzaa Sheshani, na Sheshani akamzaa Alai.

32. Yada, nduguye Shamai, alikuwa na wana wawili: Yetheri na Yonathani. Lakini Yetheri alifariki bila watoto.

33. Yonathani alikuwa na wana wawili: Pelethi na Zaza. Wote hao ni wazawa wa Yerameeli.

34. Sheshani hakuwa na watoto wa kiume; alikuwa na binti tu. Hata hivyo, alikuwa na mtumwa wa Kimisri, jina lake Yarha.

35. Hivyo, Sheshani akamwoza Yarha mtumwa wake, mmoja wa binti zake, naye akamzalia mwana jina lake Atai.

36. Atai alimzaa Nathani, Nathani akamzaa Zabadi.

37. Zabadi akamzaa Eflali, Eflali akamzaa Obedi,

38. Obedi akamzaa Yehu, Yehu akamzaa Azaria,

39. Azaria akamzaa Helesi, Helesi akamzaa Eleasa,

40. Eleasa akamzaa Sismai, Sismai akamzaa Shalumu,

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 2