Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 2:28-35 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Wana wa Onamu walikuwa Shamai na Yada. Nao wana wa Shamai walikuwa Nadabu na Abishuri.

29. Abishuri alioa mke, jina lake Abihaili, naye akamzalia wana wawili: Abani na Molidi.

30. Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu; lakini Seledi alifariki bila watoto.

31. Apaimu alikuwa na mwana mmoja aliyeitwa Ishi. Ishi alimzaa Sheshani, na Sheshani akamzaa Alai.

32. Yada, nduguye Shamai, alikuwa na wana wawili: Yetheri na Yonathani. Lakini Yetheri alifariki bila watoto.

33. Yonathani alikuwa na wana wawili: Pelethi na Zaza. Wote hao ni wazawa wa Yerameeli.

34. Sheshani hakuwa na watoto wa kiume; alikuwa na binti tu. Hata hivyo, alikuwa na mtumwa wa Kimisri, jina lake Yarha.

35. Hivyo, Sheshani akamwoza Yarha mtumwa wake, mmoja wa binti zake, naye akamzalia mwana jina lake Atai.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 2