1. Israeli alikuwa na wana wa kiume kumi na wawili: Reubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Zebuluni,
2. Dani, Yosefu, Benyamini, Naftali, Gadi na Asheri.
3. Wana wa Yuda waliozaliwa na Bethshua, mkewe Mkanaani, walikuwa Eri, Onani na Shela. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu mbele ya Mwenyezi-Mungu, basi Mwenyezi-Mungu akamuua.
4. Na Tamari, mkwewe, alimzalia wana wawili: Peresi na Zera. Jumla, wana wa Yuda walikuwa watano.
5. Peresi alikuwa na wana wawili: Hesroni na Hamuli.
6. Zera nduguye alikuwa na wana watano: Zimri, Etheni, Hemani, Kalkoli na Dara.
7. Mwana wa Karmi, alikuwa Akari. Huyu aliwaletea Waisraeli taabu kwa sababu alijiwekea nyara zilizokuwa zimewekwa wakfu.
8. Ethani alikuwa na mwana mmoja, jina lake Azaria.