Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 2:1-20 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Israeli alikuwa na wana wa kiume kumi na wawili: Reubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Zebuluni,

2. Dani, Yosefu, Benyamini, Naftali, Gadi na Asheri.

3. Wana wa Yuda waliozaliwa na Bethshua, mkewe Mkanaani, walikuwa Eri, Onani na Shela. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu mbele ya Mwenyezi-Mungu, basi Mwenyezi-Mungu akamuua.

4. Na Tamari, mkwewe, alimzalia wana wawili: Peresi na Zera. Jumla, wana wa Yuda walikuwa watano.

5. Peresi alikuwa na wana wawili: Hesroni na Hamuli.

6. Zera nduguye alikuwa na wana watano: Zimri, Etheni, Hemani, Kalkoli na Dara.

7. Mwana wa Karmi, alikuwa Akari. Huyu aliwaletea Waisraeli taabu kwa sababu alijiwekea nyara zilizokuwa zimewekwa wakfu.

8. Ethani alikuwa na mwana mmoja, jina lake Azaria.

9. Wana wa Hesroni walikuwa Yerameeli, Ramu na Kelubai.

10. Ramu alimzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Nashoni, mkuu wa kabila la Yuda.

11. Nashoni alimzaa Salma, Salma akamzaa Boazi,

12. Boazi akamzaa Obedi, Obedi akamzaa Yese.

13. Yese aliwazaa Eliabu, mwanawe wa kwanza, wa pili Abinadabu, wa tatu Shimea,

14. wa nne Nethaneli, wa tano Radai,

15. wa sita Osemu na wa saba Daudi.

16. Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa watatu: Abishai, Yoabu na Asaheli.

17. Abigaili alimzaa Amasa ambaye baba yake alikuwa Yetheri, Mwishmaeli.

18. Kalebu, mwana wa Hesroni, kutokana na wake zake wawili, Azuba na Yeriothi, aliwazaa Yesheri, Shaobabu na Ardoni.

19. Azuba alipofariki, Kalebu alimwoa Efratha aliyemzalia Huri.

20. Huri alimzaa Uri, naye Uri akamzaa Besaleli.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 2