Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 17:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Wakati mfalme Daudi alipokuwa akikaa katika ikulu, siku moja alimwita nabii Nathani, na kumwambia, “Hebu tazama, mimi ninakaa kwenye nyumba nzuri iliyojengwa kwa mwerezi, lakini sanduku la agano la Mwenyezi-Mungu linakaa hemani.”

2. Nathani akamwambia Daudi, “Fanya chochote unachofikiria moyoni mwako, kwa kuwa Mungu yu pamoja nawe.”

3. Lakini usiku uleule, neno la Mwenyezi-Mungu lilimjia Nathani, kusema,

4. “Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Mwenyezi-Mungu anasema hivi: Wewe hutanijengea nyumba ya kukaa.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 17