Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 16:3-21 Biblia Habari Njema (BHN)

3. na akawagawia Waisraeli wote, wanaume kwa wanawake, kila mmoja akapewa mkate, kipande cha nyama na mkate wa zabibu.

4. Zaidi ya hayo, Daudi aliwateua baadhi ya Walawi wawe wahudumu wa sanduku la Mwenyezi-Mungu, wamtukuze, wamtolee shukrani na wamsifu Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli.

5. Alimchagua Asafu kuwa kiongozi wao, akisaidiwa na Zekaria. Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Metithia, Eliabu, Benaya, Obed-edomu na Yehieli, aliwachagua wawe wapiga vinanda na vinubi. Asafu alipiga matoazi,

6. nao makuhani Benania na Yaharieli, walichaguliwa wawe wakipiga tarumbeta mfululizo mbele ya sanduku la agano la Mungu.

7. Basi, hiyo ikawa siku ambayo kwa mara ya kwanza, Daudi alimpa Asafu na ndugu zake Walawi wajibu wa kumwimbia Mwenyezi-Mungu nyimbo za shukrani.

8. Mpeni shukrani Mwenyezi-Mungu,tangazeni ukuu wake,yajulisheni mataifa mambo aliyoyatenda!

9. Mshangilieni, mwimbieni Mungu sifa;simulieni matendo yake ya ajabu!

10. Jisifieni jina lake takatifu;wenye kumcha Mwenyezi-Mungu na wafurahi.

11. Mwendeeni Mwenyezi-Mungu mwenye nguvu;mwendeeni Mwenyezi-Mungu daima.

12. Kumbukeni matendo ya ajabu aliyotenda,maajabu yake na hukumu alizotoa,

13. enyi wazawa wa Abrahamu, mtumishi wake,enyi wazawa wa Yakobo, wateule wake.

14. Yeye Mwenyezi-Mungu, ndiye Mungu wetu;hukumu zake zina nguvu duniani kote.

15. Yeye hulishika agano lake milele,hutimiza ahadi zake kwa vizazi elfu.

16. Hushika agano alilofanya na Abrahamu,na ahadi aliyomwapia Isaka.

17. Alimthibitishia Yakobo ahadi yake,akamhakikishia agano hilo la milele.

18. Alisema: “Nitawapeni nchi ya Kanaani,nayo itakuwa mali yenu wenyewe.”

19. Idadi yenu ilikuwa ndogo,mlikuwa wachache na wageni katika nchi ya Kanaani,

20. mkitangatanga toka taifa hadi taifa,kutoka nchi moja hadi nchi nyingine,

21. Mungu hakumruhusu mtu yeyote awadhulumu;kwa ajili yao aliwaonya wafalme:

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 16