29. Mpeni Mwenyezi-Mungu heshima ya utukufu wa jina lake;leteni tambiko na kuingia nyumbani mwake.Mwabuduni Mwenyezi-Mungu patakatifuni pake.
30. Ee dunia yote; tetemeka mbele yake!Ameuweka ulimwengu imara, hautatikisika.
31. Furahini enyi mbingu na dunia!Yaambieni mataifa, “Mwenyezi-Mungu anatawala!”
32. Bahari na ivume, pamoja na vyote vilivyomo!Furahini enyi mashamba na vyote vilivyomo!
33. Ndipo miti yote msituni itaimba kwa furahambele ya Mwenyezi-Mungu anayekujanaam, anayekuja kuihukumu dunia.
34. Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema,kwa maana fadhili zake zadumu milele!