Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 16:29-34 Biblia Habari Njema (BHN)

29. Mpeni Mwenyezi-Mungu heshima ya utukufu wa jina lake;leteni tambiko na kuingia nyumbani mwake.Mwabuduni Mwenyezi-Mungu patakatifuni pake.

30. Ee dunia yote; tetemeka mbele yake!Ameuweka ulimwengu imara, hautatikisika.

31. Furahini enyi mbingu na dunia!Yaambieni mataifa, “Mwenyezi-Mungu anatawala!”

32. Bahari na ivume, pamoja na vyote vilivyomo!Furahini enyi mashamba na vyote vilivyomo!

33. Ndipo miti yote msituni itaimba kwa furahambele ya Mwenyezi-Mungu anayekujanaam, anayekuja kuihukumu dunia.

34. Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema,kwa maana fadhili zake zadumu milele!

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 16