Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 16:25-29 Biblia Habari Njema (BHN)

25. Maana Mwenyezi-Mungu ni mkuu, anasifika sanaanastahili kuheshimiwa kuliko miungu yote.

26. Miungu yote ya mataifa mengine si kitu;lakini Mwenyezi-Mungu aliziumba mbingu.

27. Utukufu na fahari vyamzunguka,nguvu na furaha vyajaza hekalu lake.

28. Mpeni Mwenyezi-Mungu, heshima enyi jamii zote za watu,naam, kirini utukufu na nguvu yake.

29. Mpeni Mwenyezi-Mungu heshima ya utukufu wa jina lake;leteni tambiko na kuingia nyumbani mwake.Mwabuduni Mwenyezi-Mungu patakatifuni pake.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 16