Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 16:23-32 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Mwimbieni Mwenyezi-Mungu, ulimwengu wote.Tangazeni kila siku matendo yake ya wokovu.

24. Yatangazieni mataifa utukufu wake,waambieni watu wote matendo yake ya ajabu.

25. Maana Mwenyezi-Mungu ni mkuu, anasifika sanaanastahili kuheshimiwa kuliko miungu yote.

26. Miungu yote ya mataifa mengine si kitu;lakini Mwenyezi-Mungu aliziumba mbingu.

27. Utukufu na fahari vyamzunguka,nguvu na furaha vyajaza hekalu lake.

28. Mpeni Mwenyezi-Mungu, heshima enyi jamii zote za watu,naam, kirini utukufu na nguvu yake.

29. Mpeni Mwenyezi-Mungu heshima ya utukufu wa jina lake;leteni tambiko na kuingia nyumbani mwake.Mwabuduni Mwenyezi-Mungu patakatifuni pake.

30. Ee dunia yote; tetemeka mbele yake!Ameuweka ulimwengu imara, hautatikisika.

31. Furahini enyi mbingu na dunia!Yaambieni mataifa, “Mwenyezi-Mungu anatawala!”

32. Bahari na ivume, pamoja na vyote vilivyomo!Furahini enyi mashamba na vyote vilivyomo!

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 16