20. mkitangatanga toka taifa hadi taifa,kutoka nchi moja hadi nchi nyingine,
21. Mungu hakumruhusu mtu yeyote awadhulumu;kwa ajili yao aliwaonya wafalme:
22. “Msiwaguse wateule wangu;msiwadhuru manabii wangu!”
23. Mwimbieni Mwenyezi-Mungu, ulimwengu wote.Tangazeni kila siku matendo yake ya wokovu.
24. Yatangazieni mataifa utukufu wake,waambieni watu wote matendo yake ya ajabu.
25. Maana Mwenyezi-Mungu ni mkuu, anasifika sanaanastahili kuheshimiwa kuliko miungu yote.
26. Miungu yote ya mataifa mengine si kitu;lakini Mwenyezi-Mungu aliziumba mbingu.
27. Utukufu na fahari vyamzunguka,nguvu na furaha vyajaza hekalu lake.
28. Mpeni Mwenyezi-Mungu, heshima enyi jamii zote za watu,naam, kirini utukufu na nguvu yake.
29. Mpeni Mwenyezi-Mungu heshima ya utukufu wa jina lake;leteni tambiko na kuingia nyumbani mwake.Mwabuduni Mwenyezi-Mungu patakatifuni pake.
30. Ee dunia yote; tetemeka mbele yake!Ameuweka ulimwengu imara, hautatikisika.
31. Furahini enyi mbingu na dunia!Yaambieni mataifa, “Mwenyezi-Mungu anatawala!”
32. Bahari na ivume, pamoja na vyote vilivyomo!Furahini enyi mashamba na vyote vilivyomo!
33. Ndipo miti yote msituni itaimba kwa furahambele ya Mwenyezi-Mungu anayekujanaam, anayekuja kuihukumu dunia.
34. Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema,kwa maana fadhili zake zadumu milele!
35. Mwambieni Mwenyezi-Mungu:Utuokoe, ee Mungu wa wokovu wetu,utukusanye pamoja na kutuokoa kutoka kwa mataifa,tupate kulisifu jina lako takatifu,kuona fahari juu ya sifa zako.
36. Asifiwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli,tangu milele na hata milele!Kisha watu wote wakasema, “Amina!” Pia wakamsifu Mwenyezi-Mungu.
37. Hivyo, mfalme Daudi akawaacha Asafu na nduguze Walawi mahali walipoliweka sanduku la agano la Mwenyezi-Mungu, kwa ajili ya huduma zinazotakiwa mbele ya sanduku kila siku.
38. Obed-edomu, mwana wa Yeduthuni, pamoja na wenzake sitini na wanane waliwasaidia. Obed-edomu mwana wa Yeduthuni na Hosa walikuwa walinzi wa malango.