Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 16:13-20 Biblia Habari Njema (BHN)

13. enyi wazawa wa Abrahamu, mtumishi wake,enyi wazawa wa Yakobo, wateule wake.

14. Yeye Mwenyezi-Mungu, ndiye Mungu wetu;hukumu zake zina nguvu duniani kote.

15. Yeye hulishika agano lake milele,hutimiza ahadi zake kwa vizazi elfu.

16. Hushika agano alilofanya na Abrahamu,na ahadi aliyomwapia Isaka.

17. Alimthibitishia Yakobo ahadi yake,akamhakikishia agano hilo la milele.

18. Alisema: “Nitawapeni nchi ya Kanaani,nayo itakuwa mali yenu wenyewe.”

19. Idadi yenu ilikuwa ndogo,mlikuwa wachache na wageni katika nchi ya Kanaani,

20. mkitangatanga toka taifa hadi taifa,kutoka nchi moja hadi nchi nyingine,

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 16