Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 16:1-11 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kisha waliliingiza sanduku la Mungu, na kuliweka ndani ya hema ambayo Daudi alikuwa ameitayarisha. Halafu wakatoa tambiko za kuteketezwa na za amani mbele ya Mungu.

2. Daudi alipomaliza kutoa tambiko hizo za kuteketezwa na za amani, aliwabariki watu katika jina la Mwenyezi-Mungu,

3. na akawagawia Waisraeli wote, wanaume kwa wanawake, kila mmoja akapewa mkate, kipande cha nyama na mkate wa zabibu.

4. Zaidi ya hayo, Daudi aliwateua baadhi ya Walawi wawe wahudumu wa sanduku la Mwenyezi-Mungu, wamtukuze, wamtolee shukrani na wamsifu Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli.

5. Alimchagua Asafu kuwa kiongozi wao, akisaidiwa na Zekaria. Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Metithia, Eliabu, Benaya, Obed-edomu na Yehieli, aliwachagua wawe wapiga vinanda na vinubi. Asafu alipiga matoazi,

6. nao makuhani Benania na Yaharieli, walichaguliwa wawe wakipiga tarumbeta mfululizo mbele ya sanduku la agano la Mungu.

7. Basi, hiyo ikawa siku ambayo kwa mara ya kwanza, Daudi alimpa Asafu na ndugu zake Walawi wajibu wa kumwimbia Mwenyezi-Mungu nyimbo za shukrani.

8. Mpeni shukrani Mwenyezi-Mungu,tangazeni ukuu wake,yajulisheni mataifa mambo aliyoyatenda!

9. Mshangilieni, mwimbieni Mungu sifa;simulieni matendo yake ya ajabu!

10. Jisifieni jina lake takatifu;wenye kumcha Mwenyezi-Mungu na wafurahi.

11. Mwendeeni Mwenyezi-Mungu mwenye nguvu;mwendeeni Mwenyezi-Mungu daima.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 16