Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 14:3-10 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Huko Yerusalemu, Daudi alioa wake wengi zaidi, naye akazaa wana na mabinti wengine.

4. Yafuatayo ndio majina ya watoto aliozaa huko Yerusalemu: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni,

5. Ibhari, Elishua, Elpeleti,

6. Noga, Nefegi, Yafia,

7. Elishama, Beeliada na Elifeleti.

8. Wafilisti waliposikia kwamba Daudi amepakwa mafuta kuwa mfalme wa nchi nzima ya Israeli, wote walitoka kwa wingi kwenda kumtafuta. Daudi alipopata habari, alitoka kwenda kuwakabili.

9. Wafilisti walifika wakaanza mashambulizi katika bonde la Refaimu.

10. Ndipo Daudi alipomwuliza Mungu shauri, “Je, niende kuwashambulia Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Naye Mwenyezi-Mungu akamwambia, “Nenda, nitawatia mikononi mwako.”

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 14