Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 14:13-17 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Kisha Wafilisti walifanya mashambulizi katika bonde hilo kwa mara ya pili.

14. Safari hii, Daudi alipoomba shauri kwa Mungu, Mungu akamwambia, “Usiwashambulie kutoka hapa, ila zunguka na kuwashambulia kutoka mkabala na miti ya miforosadi, halafu washambulie kutoka huko.

15. Na mara utakaposikia vishindo vya gwaride kwenye vilele vya hiyo miforosadi, haya, toka uende vitani. Nitakuwa nimekwisha kukutangulia kulipiga jeshi la Wafilisti.”

16. Daudi alifanya kama alivyoamriwa na Mungu. Alilipiga jeshi la Wafilisti kutoka Gibeoni hadi Gezeri.

17. Daudi akawa maarufu kote nchini, naye Mwenyezi-Mungu akayatia hofu mataifa yote, nayo yakamwogopa sana.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 14